Jumamosi, 24 Septemba 2016

PALILIA IMANI YAKO



Inatakiwa niipalilie imani yangu kwa sababu imani yangu ndio msaada wa maisha yangu, vilevile Imani niliyo nayo nikiipalilia vizuri ndio itakayo nisaidia kupata utawala wa rohoni, na ndicho kinachotakiwa kwa mkristo anayemwamini Yesu Kristo.

ANGALIZO NO. 1 :
      • Majaribu yaliyonizunguka yataondoka kwangu kadri Imani     yangu inavyokua .

      • Namna ambavyo naweza kuipalilia Imani yangu ikawa na mizizi ambayo itanisaidia kukabiliana na changamoto yoyote ile ni kuruhusu moyo wangu uelimishwe na Neno la Mungu   ( Biblia ).  

       •Hii inasikitisha wakristo wengi hupuuzia kujifunza Neno la Mungu ( kusoma Biblia ) ndio maana shetani amepata uwezo wa kuwaweka waamini chini ya mgandamizo

      • Mgandamizo hauwezi kuruhusu imani ya mkristo kupokea Baraka zake kutoka kwenye uso wa Mungu, kwa sababu mgandamizo huyapofusha macho ya imani ya mkristo ,kwa hiyo ni vigumu mkristo kutambua kusudi la Mungu katika maisha yake.

       •( Macho ya imani yakipofuka mkristo ataishi chini ya utumwa wa dhambi  )

       •Mkristo aliyepofuka macho ya kiroho hawezi kuwa na ufahamu wa kutambua Baraka za Mungu zinakuja kwake kwa njia gani.

               -Jambo la kufahamu katika maisha yangu kama mwamini wakristo tuliookoka lazima tuwe makini sana tunaishi katika maisha yenye changamoto na vipingamizi vingi sana, ndio maana inatakiwa kuziendeleza roho zetu katika kumfahamu Mungu zaidi ili tupate wepesi wa kuyafikia maono yetu

       • Nisipo ruhusu roho yangu kuendelezwa na Neno la Mungu Imani yangu itapoteza ujasiri wa kukabiliana na utawala wa giza.
              - Mfano mzuri katika Biblia wa mkristo aliyepoteza utawala katika roho ( ujasiri ) ni wana wa Skewa.  Matendo ya Mitume;  19:13-16
       •Mkristo anayeishi chini ya mgandamizo ndani yake hana mamlaka yoyote ya kukabiliana na ufalme wa giza.

       •Mkristo anayeishi maisha ya dhambi maisha yake hukosa mpenyo, vilevile mwanga wa ki-Mungu Mstari wa 16,

       •Imani ya mkristo ikikosa ujasiri ni vigumu kuruhusu mpenyo wa  Baraka

       •Mkristo ambaye haishi maisha ya ukweli kila jambo mbele yake litampa utata.

       •Mwamini akiamua kuipalilia imani yake kupitia Neno la Mungu changamoto zitakazo jitokeza mbele yake hazitakuwa na nguvu.

        •Ili niweze kuvuka kila changamoto inayojitokeza mbele yangu inatakiwa niruhusu Neno la Mungu kuyaongoza maisha yangu. Yohana 5:5-9 
         •Mgandamizo ukiyakalia maisha ya mwamini, imani aliyonayo hupoteza mwelekeo yaani hata kile anachokijua anakisahau
         *(Mkristo anayeishi katika maisha ya mgandamizo kamwe hawezi kuishi maisha ya ukweli mpaka afunguliwe, na inafahamika wazi maisha ya ukweli ndio yanayo ruhusu Baraka za Mungu kuambatana na mtu. )*
          •Sauti ya Mungu ni Neno lake kwa maana zaidi ninaposoma Biblia najibishana na Yesu Kristo uso kwa uso.
          •Wakristo wa leo hawaamini kwamba Biblia ni hai katika maisha yao ndio maana kanisa la leo  halisisitizwi kabisa katika kusoma Biblia, ndio maana wakristo walio wengi wameweka tegemezi zaidi katika kuombewa kuliko kukaa chini na kujifunza neno la Mungu likampa maarifa ya kumtoa katika matatizo aliyonayo.

NIKIIPALILIA IMANI YANGU ITANIPA FAIDA ZIFUATAZO : 
A. Kutembea na Roho Mtakatifu
B. Kupata mamlaka ya Neno ( Uumbaji )
C. Nguvu ( Power )

UFAFANUZI WA VIPENGELE HAPO JUU:
A. Kutembea na Roho Mtakatifu.
     o Mkristo anayeishi maisha ya Imani ndiye mwenye uwezo wa kutembea na Roho Mtakatifu kwa sababu mwamini wa aina hiyo anakuwa anaishi sambamba na mapenzi ya Mungu.
     o Roho Mtakatifu anajifunua kwa mkristo mwenye kina cha Neno la Mungu.
     o Nikiwa Mkristo nisiyekuwa na kina cha Neno ninakuwa ni Mkristo kimwili lakini kiroho sio Mkristo.
     o Mwamini anayetambulikana kwamba ni Mkristo katika roho ni Yule ambaye maisha yake anayaendesha kama Neno la Mungu linavyosema hata kitabu cha Warumi kimesisitiza . WARUMI 8: 13- 16,  

ANGALIZO NO. 2
     o Mkristo mwamini akiishi kwa kufuata maumbile ya kibinadamu yaani mapenzi ya mwili hawezi kuungana na Baraka za Mungu, kwa sababu Mungu kuna kitu amesema katika kitabu cha Wakorinto.
      o 1 wakorinto 6 : 17  -( Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye ).
Nini maana ya kuungwa na Bwana kama inavyosema  1kor 6:17 ?
      • Maana ya kuungwa na Bwana ni kuyafanya maisha yangu yakae chini ya muongozo wa neno la Mungu maana yake Biblia.
Wakristo  waamini  tunapata nguvu ya Mungu kupitia Neno ( Biblia).
Neno la Mungu ndilo linalompa mkristo mwamini nguvu( uwezo ) wa kukabiliana na ufalme wa giza

( Mkristo atakaye mwuona  Mungu ni Yule atakayeweka mizizi katika Neno la Mungu).
Katika kufundishwa Neno la Mungu(Biblia ) ninapata faida ya upeo wa ufahamu wangu kuongezeka ,kwahiyo itanisaidia namna ya kuambatana na Baraka za Mungu.
Nguvu ya Mungu inajiumba kwa mkristo ambaye ameamua kuutia moyo wake ufahamu wa kufundishwa Neno la Mungu.
( Nikiwa kwenye uwepo wa Mungu nahitaji kuwa na uhalisia wa kile kinacho tamkwa ndipo nitafanikiwa).
Wakristo wengi wanaokuwa kwenye uwepo  wa Mungu wanapoteza uhalisia  wa kupokea Baraka zao kwasababu misingi ya imani yao imejijenga katika vinavyoonekana.
Biblia ni nguvu ya mkristo anayemwamini Yesu Kristo.
Mkristo anayesoma Neno la Mungu katika imani lile neno linakuwa hai kwake kwahiyo hata atakapo kutana na majaribu atapata wepesi wa kupenya kwasababu nyuma yake kuna nguvu ya Neno la Mungu.
Mkristo aliyelifanya Neno la Mungu kuwa sehemu ya maisha yake  akawa analisoma katika misingi ya kiimani akaliheshimu na kuliamini  hila  yoyote ya shetani haiwezi  kumsogelea kwasababu Neno la Mungu humfunua shetani na kumuacha uchi mbele ya  macho ya mkristo anayeliamini Neno la Mungu Waebrania 4:12.
Ninapolisoma Neno la Mungu moyoni mwangu ninajengeka katika  nguvu za kiroho,kwahiyo kila jambo nitakalolifanya  au nitakalolikusudia moyo wangu utanipa ishara kwamba ni sahihi au si sahihi.
Wakristo wengi wametumia nguvu  nyingi sana katika kujiharibu, tena sanasana jamii ya waaminio ,kuliko kutumia nguvu nyingi kujijenga katika imani.
Mkristo akifundishwa Neno akapata nguvu za rohoni shetani hawezi kupata nafasi ya kuingiza uvamizi.
Nguvu inakuja katika moyo wa mwamini kadri mwamini anavyoongeza juhudi ya kulisoma Neno la Mungu
Zaburi 119:11
Madhaifu yanaingia katika maisha ya wakristo ,kwasababu mioyo yao inakuwa tayari imepoteza nguvu ya Neno la Mungu.
Moyo wa mkristo ambao umepoteza nguvu ya neno  tabia za mwilini yaani za kimwili huanza kujidhihirisha.
Nikiona tabia Fulani ya kimwili inaambatana na mimi au inanisumbua sana inatakiwa niongeze juhudi katika kusoma  Biblia na kufundishwa Neno la Mungu hapo nitapata mpenyo wa ushindi.
Tabia yoyote iliyofungamana na maisha ya mtu isiyompendeza Mungu ili iweze kun’gooka inatakiwa roho ya mtu huyo ielimishwe na Neno la Mungu  kwelikweli  kwasababu tabia haina tofauti na roho chafu, ndio maana Biblia Zaburi  119:9 imetoa siri ya ushindi.
Njia ya kuyafanya maisha yangu ya wokovu yawe safi ni namna nitakavyokuwa na juhudi katika kujifunza Neno la Mungu , hii husaidia zaidi kuyafanya maisha ya  mwamini kuwa karibu na uwepo wa Mungu.
FAIDA YA NGUVU YA NENO:
Moyo wa mwamini  ukiimarika katika Neno la Mungu ndani mwake  huzaliwa imani yenye uwezo wa kuumba ,jambo hili lilimkuta Petro na Yohana wakielekea hekaluni .
Matendo ya Mitume 3:1-.
Katika Matendo ya Mitume 3:4. Kuna kipengele ambacho Petro alisema “ tutazame sisi”  alikuwa akidhihirisha wazi nguvu ya Neno la Mungu iliyojawa ndani mwake.
( Kupokea kwa mkristo anayemwamini Yesu Kristo kunaanzia katika Roho).
Hata kitendo cha kutokuliamini Neno la Mungu ni uzinzi tayari.
Maisha ya wokovu nilionao yatakuwa salama  kama nikiweka jitihada za kutosha za kufundishwa Neno la Mungu ,faida nitakayoipata katika hilo maisha yangu yatakuwa chini ya uwepo halisi wa Kimungu  


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni