SOMO: UNAHITAJIKA (YOU ARE NEEDED)
Mathayo 9:37-38 Mavuno
ni mengi watendakazi ni wachache.
ISAYA 6:8
Nimtume Nani ?
Dunia hii imejaa
mambo mengi yanayohitaji watu wa Mungu
kuyarekebisha .Baada ya anguko la Adamu na Hawa Mwanadamu alipoteza nafasi
kubwa na Kumiliki ,kutawala na kutiisha kama alivyokuwa amepewa na Mungu
awali.mamlaka hiyo ilichukuliwa na Ibilisi shetani baada ya kufaulu kumdanganya
na kumtenga Adam na Mungu.Uhusiano wa Mungu na Adam ulikorofishwa ndiposa laana
ilianza kumpata na kuishi maisha yenye majuto ,taabu na dhiki.
Mwana wa Mungu Yesu
Kristo alipokuja alirejesha ile mamlaka ya Adam kupitia ukombozi kwa Damu yake
na mamlaka hiyo alituachia sisi tuliozaliwa mara ya pili.
Hivyo wewe
uliyezaliwa kwa Mara ya pili ,wewe ni mtu wa thamani sana ,UNAHITAJIKA katika
dunia hii kufanya mambo kadha wa kadha katika kurejesha Ufalme wa Mungu hapa
Duniani.Hali iko hivi:
Dunia imejaa watu :
a)
Wanaoangamizwa na shetani kwa kukosa
maarifa Hosea 4:6
b)
Wasiomjua Mungu wa kweli ni yupi ,
waliopotea kabisa
c)
Wenye kukata tamaa ya maisha ,wasio na matumaini tena
d)
Waliovunjika mioyo
e)
Waliosetwa
f)
Wenye kujaa ujinga wa kila namna ,wamepandikizwa
roho ya uasi
g)
Ndugu ,jamaa na marafiki wenye
kufungwa kiroho na za kimwili
h)
Wenye kupagawa na nguvu za giza wanaohitaji
msaada wa ukombozi
i)
Wenye kupotea dhambini na hawana mtu
wa kuwapelekea Habari njema ya Wokovu
j)
Wanaoonewa na shetani na kukandamizwa
kabisa ,hawafurukuti maana wamepofushwa akili zao na ibilisi shetani.
k)
Wamefungwa
kihisia,kisaikolojia,kiakili,kiroho na kimwili.
l)
Wasiojua nini cha kufanya ili
kuondokana na hali zao zenye kutisha na kuhuzunisha nk….
Hivyo ndugu yangu Tambua
kwamba UNAHITAJIKA !
Mwana wa Mungu popote
ulipo ,chochote unachokifanya ,fahamu kwamba wewe UNAHITAJIKA !
Hivyo usibweteke
,usilale ,usijisahau ,okoa jahazi watu
wanaangamia.
Kumbuka “una hazina
kubwa sana ndani yako inayoweza kuzaa matunda makubwa mno “
a)
Una uwezo wa kulisha maelfu
b)
Una uwezo wa kumuondoa mtu kifungoni
c)
Una uwezo wa kupindua mipango na hila
za ibilisi
d)
Ukisimama kwenye zamu yako una uwezo
kwa kufanya mambo yasiyo ya kawaida wakati ungali unaishi katika hali ya
kawaida .Ndiyo maana Yesu anasema Ishara hizi zitamambatana na hao waaminio ,Amwaminiye atatenda zaidi ya yale ambayo
hakutenda.
Unahitajika
ü kufanya
kitu hapa dunani kwa ajili ya Bwana
ü kusaidia
hao watu waliotajwa hapo juu kubadili hali ya mambo
Mungu amekupa elimu
uliyo nayo kwa makusudi .Elimu yoyote njema uliyo nayo (ya kiroho au ya kimwili)
,Mungu amewekeza ndani yako akitarajia kuwa na wewe utaitumia kusaidia
wanaoihitaji na kwamba utaimbaza kwa wengine.
Hata Wazazi
wamekusomesha wakitegemea kuja kusaidiwa na wewe baadaye.Unahitajika
kuwarejeshea matumaini mazuri siyo mambo ya kuhuzunisha au kusikitisha .
Una hazina kubwa
inayoweza kumsaidia jirani aliye karibu na wewe na aliye mbali.Ndiyo maana Yesu
anasema Umpende Jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe maana yake umhudumie
kadiri uwezavyo ukitumia hazina uliopewa kam tunu ya mabadiliko ya aina yoyote.
Maisha unayoishi
yamefichwa ndani ya pakeji inayoitwa kusudi.Mhubiri 3:1 “ kwa kila jambo
kuna wakati wake na kusudi chini ya jua “
Komboa wakati ili
utimize kusudi.Galatia 5:16
Uliumbwa kwa kusudi
maalum ndiyo maana hufanani na mtu yeyote duniani .Umewekewa na Mungu hazina
kubwa ndani yako ili uweze kuitumia kutimiza kusudi hilo .hazina hiyo ndiyo
inayokurahishia kutimiza kusudi la Mungu la kukuumba.KILE ULICHO NACHO ,KUNA
MTU ANAKILILIA MAANA ANAKIHITAJI HAKIKA NA WEWE UNAHITAJIKA KUMRAHISHIA
KUKIPATA APATE KUPONA.
Katika dunia hii ,Mtu
wa Mungu anahitajika katika maeneo makuu mawili :
a)
Mambo ya kiroho
b)
Mambo ya kimwili
- KIROHO
UNAHITAJIKA :
1)
KUMTUMIKIA MUNGU (TO SERVE GOD
) :
Unahitajika kutumwa na Mungu yaani
kumtumikia ISAYA 6:8 Nimtume Nani?
Mathayo
9:37-38 /Luka 10:2 Mavuno ni mengi watendakazi ni wachache.
Mifano ya watu waliohitajika wakafanya
:
ü Yesu
alihitajika kuja kukomboa wanadamu Yohana 3:16
ü Yusufu
alihitajika kukomboa familia yake
ü Ibrahimu
alihitajika kuwa Baba wa Imani wa Vizazi vyote
ü Nuhu
alihitajika kubeba kusudi na mpango wa Mungu
ü Esther
alihitajika kukomboa ukoo wake
ü Paulo
alihitajika kupeleka injili kwa wasiotahiriwa
ü Petro
alihitajika kupeleka injili kwa waliotahiriwa
Kila
mtumishi wa Mungu kwenye Biblia (Nabii,Wafalme ,Mitume…) alihitajika kufanya
kazi maalum la kumtumikia Mungu aliyoitiwa
kufanya (Musa ,Yoshua walihitajika
kuongoza wana wa Israeli Kanani )Hivyo
na wewe unahitajika kutimiza WITO wako kwa kumtumikia Mungu . Fanya kazi ya
Bwana .
2)
KULETA MABADILIKO YA KIROHO KATIKA
JAMII
a)
Kutia moyo waliovunjika Isaya 35:3-4 Itieni nguvu mioyo
iliyo dhaifu
b)
Kupoza wagonjwa ,kufufua wafu,kutakasa
ukoma Mathayo 10:8
3)
KUHUBIRI
a) Kuhubiri
injili yaani kumtangaza Kristo ( Habari njema ) duniani kote Marko 1:14
Mathayo 28:19-20
Basi ,Enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi ,mkiwabatiza kwa jina la
Baba na Mwana na Roho Mtakatifu .
Uwe tayari kwenda ! Marko
3:14
b)
Kueneza ufalme wa Mungu
4)
Kuombea kanisa , watumishi na watu
wote 1 Timotheo 2:1
5)
Kutengeneza njia ya Bwana na Kunyosha
mapito ya Bwana Mathayo 3:3
6)
Kusimama mahali palipobomoka
7)
Kuwa kielelezo katika usemi ,mwenendo
,upendo imani,usafi 1 Timotheo 4:12
8)
Kutumia karama iliyopo ndani yako 1 Timotheo 4:14
9)
Kuondoka na kuangaza Isaya 60:1
10) Kuamka
usingizini Efeso 5:14 1 Tesalonike 5:6
11) Kupiga
vita vizuri vya imani 1 Timotheo 6:12
12) Kuomba
bila kukoma 1 Tesalonike 5:17
13) Kuagiza
na kufundisha 1 Timotheo 4:11
14) Kufuata
haki ,utauwa,imani,upendo,saburi na upole 1
Timotheo 6:11
15) Kuenenda
kwa roho Galatia 5:16
16) Kusimama
imara katika Bwana Filipi 4:1
17) Kubadilika
na kubadili hali ya mambo kwa kujitenga
na ubaya wa kila namna
1 Tesalonike 5:22
18) Kusimama
kwenye zamu yako Habakuki 2:1
- KIMWILI
UNAHITAJIKA :
- Kujenga
mitazamo ya watu (People’s Mindsets transformation)
- Kusaidia
wahitaji yaani kutenda mema 1
Tesalonike 3:13
Yatima
,wajane ,wagane ,wasiyojiweza,walemavu
- Kuleta
MABADILIKO ya kimwili popote ulipo
·
Mabadiliko ya kifra : Kubadili fikra
na mitazamo ya watu kupitia kuwaelimisha
·
Mabadiliko ya kiuchumi
- Kuleta
MAENDELEO kanisani ,kwenye family na katika taifa lako
- Kusaidia
familia jamii ,marafiki na ndugu
·
Kiuchumi
·
Kimaendeleo
·
Kiafya
·
Kiakili
·
kielimu
- Kutunza
walio wa nyumbani mwako 1 Timotheo
5:8
- Kujenga
uchumi wa nchi , kwa kufanya kwa moyo kila jambo Mhubiri 9:10 Kolosai 3:23
- Kufanya
kazi kwa bidii 1 Tesalonike
3:10-11 2 Tesalonike 4:11 2 Tesalonike 3:8
Chukua
hatua sasa !
Mungu
akubariki sana !
MWALIMU
JAMES SADY 0717 820 8980
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni